Njia 7 za kuongeza wasomaji wa Blog yako

Katika ulimwengu wa leo neno blog siyo kitu kigeni, leo hii karibu kila mtumiaji wa internet anayo blog yake. Blogu hizi kuna zile zinazotembelewa na watu wengi na kuna zile zinazopata watembeleaji kwa mdondo.Je umewahi kujiuliza kwanini watu hawatembelei blog yako kama wanavofanya kwa blog fulanifulani? Ingawa kuna sababu nyingi kama umri wa blog, umarufu wa mmiliki wa blog nk lakini kuna kuna vitu ambavyo unaweza kuvifanya na vikakuongezea idadi ya watembeleaji.

Hivyo kwenye makala ya leo tutaangalia ni vitu gani vya msingi kuzingatia ili blog yako ivutie wasomaji wengi zaidi.

Whatsapp yanunuliwa na Facebook, nini tutegemee

Kama ulikuwa haufahamu, habari kuu katika ulimwengu wa Teknohama kwa siku ya leo ni Facebook kuinunua Whatsapp kwa bei ya dola bilioni 19.  Nunuzi hilo ni la programu pekee na siyo kampuni ingawa wafanyakazi wa whatsapp watajiunga na timu ya Facebook moja kwa moja, mission za whatsapp zitaendelea kubaki kama zilivyo, alieleza Jan Koum ambaye ni muanzilishi wa whatsapp.

Kwa wasio fahamu, whatsapp ni moja ya programu ya simu za mkononi inayokuwezesha kutuma ujumbe wa simu kupitia kwenye intaneti badala ya ujumbe mfupi (sms). Kwa kutumia whatsapp, inamaana utaepuka gharama za sms huku ikiwa imesheheni matumizi mengine mengi zaidi kama kutuma picha, sauti uliyojirekodi nk.

Hadi sasa, whatsapp ina watumiaji hai milioni 450 kila mwezi kutoka nchi nyingi duniani, huku kukiwa na watumiaji wapya zaidi ya milioni moja kila siku. Hivyo, ni dhahiri kuwa whatsapp ni programu pendwa na yenye kutumika.

Mambo 5 ya kuzingatia juu ya matumizi ya Mitandao ya jamii

Siku hizi, katika kila watu kumi wanaotumia mtandao, basi angalau watano kati ya hao wanatumia mitandao jamii. Kuna baadhi ya watu wamegeuza mitandao hii kuwa kama ni sehemu ya mawasiliano, ama ya mtu kwa mtu au ya kibiashara. Siku hizi, si kitu cha kushangaza kusikia mtu maarufu au kiongozi fulani atakuwa kwenye Facebook saa fulani kwa ajili ya kujibu maswali ya wananchi / mashabiki wake. Mitandao hii ni kama vile Facebook, Twitter, Jamiiforums nk, hivyo basi, hatuwezi kuepuka ushawishi wa mitandao jamii katika jamii yetu.

Matumizi bora ya mitandao jamii huweza kuleta faida nzuri sana, ila huwa kinyume pale inapotumika sivyo, ama kwa kutokujua ama kwa kuamua. Hivyo leo hii tuangalie mambo kadhaa ya kuepuka unapotumia mitandao jamii.

1. Epuka kujiacha wazi kwenye mitandao jamii.

Makosa makuu 3 wanayokutana nayo kwa wingi watumiaji wa website na maana zake

Kama wewe ni mtumiaji wa website, basi moja ya vitu vinavyokera ni pale unapofungua website halafu haifunguki. Kutofunguka kwa website kunaweza kusababishwa na matatizo mengi. Kuna matatizo ambayo yanaweza kuwa ni upande wako wewe 

mtumiaji kama (intaneti yako kuwa chini sana, au programu ya ulinzi (anti virus) inakuzuia kufungua hiyo website nk, pia inaweza kuwa ni tatizo la website husika. Ili kuweza kusaidia kutambua chanzo cha tatizo na kurahisisha matumizi, kila kosa linalotokea kwenye website limepewa namba husika ambayo italitambulisha, ama kwa watumiaji ama kwa wamiliko na hii tunaiita namba ya utambulishi wa error (error status code) .

Kuna rundo la makosa unayoweza kukunana nayo, ila leo hii tutaangalia yale yanayotokea mara kwa mara;

Jinsi ya kupima mafanikio ya website - Sehemu 2

Katika sehemu ya kwanza ya jinsi ya kupima mafanikio ya Website, tumeangalia dhumuni la upimaji wa mafanikio, pia tumeangalia vitu muhimu vya kuzingatia. Tumeona umuhimu wa kuwa na malengo yenye sifa kuu tano au kwa kifupi (SMART).

Katika sehemu hii ya pili, tutaangalia vizio muhimu vya upimaji wa mafanikio ya Website.

Kama tunavyojua, dhumuni la kuwa na website ni ili iweze kutumika kwa watu, wawe wateja, wafanyakazi au hata washirika. Kwa kujua takwimu za matumizi ya watu hawa, ni dhahiri utaweza kujua ufanisi wa Website yako. Vizio hivi vya
uchambuzi vitakuwezesha kupata picha kamili ya ni jinsi watu wanafika vipi kwenye website yako, wakifika wanatembelea kurasa gani, wanakaa muda gani nk. Google analytics ni moja ya website ambazo zinaweza kukusaidia kupata takwimu hizi.

Hebu, tuangalie vizio hivi;

Jinsi ya kupima mafanikio ya Website yako - Sehemu 1

Katika makala zilizopita tumeangalia umuhimu wa kuwa na Website. Pia tumeangalani hatua muhimu za kupitia mpaka unakuwa na website. Lengo la website ni kufanya kazi na siku ya mwisho wewe kama mmiliki ni lazima uone matokeo ya kazi iliyofanywa na website.

Ingawa kumekuwa na mijadala sana kwenye uwanja wa IT juu ya upimaji wa matokeo ya IT, wengi wakisema, ni ngumu kupima matokeo yanayosababishwa na IT pale ambapo IT inakuwa ni  muwezeshaji, na website ikiwa ni sehemu moja wapo. Ukweli ni kuwa, kwa sasa IT si muwezeshaji tena, bali ni sehemu ya kazi. Hivyo, inatakiwa itoe matokeo tena yanayopimika, na website ni sehemu mojawapo. Na lazima ijumuishwe kwenye malengo ya kampuni / shirika.

Kitendo cha upimaji wa Website hutegemea na sababu ya kuanzishwa kwake, leo hii kuna mamia ya website kwenye kila idara, kuanzia blogu za habari hadi zile website za serikali. Hivyo hakuna njia moja kupima mafanikio hayo. Kwakuwa kila website ina malengo tofauti, lakini kuna kitu ambacho website zote zinahusika, nacho ni; zote zinamlenga mtumiaji na mmiliki.

Mazingatio 10 juu ya majina ya website

Je umeshawahi kufikiria ni jinsi gani watu wananyohangaika kufika mtaani kwenu kama huo mtaa jina lake halieleweki au kukumbukika kirahisi? Chukulia mtaa wenu unaitwa "Kwa mporomosha matikiti", siyo tu hili jina ni refu, bali linajumuisha maneno ambayo yanachanganya sana "mporomosha" kwani sisi wengine tutaita "mpolomosha".

Majina ya Website ama kwa kingereza wanaita "Domain Names", kama ilivyo anuani za mitaa au nyumba zina maana kubwa sana kwenye ulimwengu wa Website. Uchaguzi wake ni moja ya vitu muhimu sana katika maisha ya website, jina lisiloeleweka, siyo tu litaweza kumpa faida mpinzani wako, bali kuwachanganya wateja na hivyo kupunguza kasi ya ukuaji wako kwenye mtandao.

Kabla hatujaendelea, lazima tujue ni kwa nini kuna majina ya website?

Connect With Us

 

New Project?

We do not just put codes to make a system, we help companies in their digital transformation challenges. We automate business process, workflows and communication.

Image