JOOMLA! CMS WEBSITE / BLOG DESIGN & MAINTENANCE BOOT CAMP

JOOMLA! CMS WEBSITE / BLOG DESIGN & MAINTENANCE BOOT CAMP

November 8,9,15 and 16

DUDUMIZI TECHNOLOGIES LTD, Website design and Development Company in Tanzania is organizing 4 days  (2 Saturdays and 2 Sundays) training to equip participants with the skills, knowledge and techniques of designing, developing and maintaining good websites / blog by using Open source Content Management System called Joomla! 

Joomla is an award-winning content management system (CMS), which enables people to build Websites and powerful online applications. Joomla the most popular Websites software in the world. Almost 80% of Websites in Tanzania are designed using Joomla. 

Umuhimu wa vipimo na takwimu ili kuboresha biashara

Katika dunia hii ya utandawazi, ushindani ni kitu kisichoepukika. Haijarishi wewe unafanya biashara ya kuuza peni au una blogu yako au hata unauza dhahabu. Utandawazi umeweza kuwafanya wanunuzi wawe na sauti na machaguo mengi toka kila pande, pande hizi zinaweza kuwa hata nje ya mipaka ya nchi. Pia, wanunuzi wamepewa uwanja mkubwa wa kuijadili na kupata taarifa za biashara yako kwa urahisi zaidi, mitandao jamii ni moja ya kitendea kazi kwenye hili.

Ingawa ushindani ni mkubwa sanasana, lakini leo hii, kama utatembelea kwenye biashara kadhaa nchini Tanzania, utakubaliana na mimi kuwa, wengi tunafanya biashara kwa mazoea (business as usual)na ubunifu umekuwa mdogo sana kwa makampuni mengi sana. Iwe ya serikali au hata ya watu binafsi, iwe madogo yaliyoanza jana au hata yale yenye umri wa miongo.

KITABU: Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara

Mitandao jamii imekuwa moja ya nyenzo imara kabisa ya kujitangaza na kuwafikia walengwa wengi kwa uharaka na mapana zaidi kwa njia ya mtandao. Jiulize swali dogo tuu, je kwa siku za karibuni umekuwa ukitumia njia gani kufahamu juu ya bidhaa au huduma fulani.

Je kwa kutumia tangazo la kwenye TV au Radio ambapo hauna uhakika hata saa ngapi wataonesha tangazo unalohitaji? Au kwa kupitia gazeti ambapo wengi wetu sasa inapita hata mwezi bila kusoma gazeti lililochapishwa? Au ni mara ngapi umetumia muda wako kusoma lundo la emails kwenye sanduku la email za matangazo (Junk emails)?

Siku hizi watu wamebadilika sana, wateja hupendelea kutafuta huduma toka mahali ambapo wanapata taarifa zote kwa upamoja tena pindi wanapohitaji, baadhi ya njia watumiazo kwa sana ni kama; kwa kutumia mitambo ya utafutaji (search engines) au toka kwa marafiki zao walio kwenye mitandao jamii (Social networks). Na huko ndiko kunakoshibisha njaa ya huduma na kujibu maswali yao yote.

Mafundisho: Matumizi sahihi ya Facebook kwa Wafanyabiashara

Katika dunia ya leo, kama wewe ni mfanyabiashara basi hauwezi epuka ushawishi wa mitandao jamii. Ingawa wengi wetu tumekuwa tukiitumia mitandao jamii kwa ajili ya mawasiliano pekee, ila kuna mengi yanaweza kufanyika na kusaidia kukuza ufannisi wa biashara yako.

Kwa kulitambua hilo, Dudumizi Technologies LTD inakuletea mafunzo juu ya njia na namna sahihi za kutumia Facebook kukuza na kuboresha Biashara.

Mafunzo haya yatakuwa ya wiki mbili, bila kukuchosha (tukitambua muda ni kitu muhimu kwa mjasiriamali), tutakutumia dondoo (kwa email fupi) iliyojikita moja kwa moja kwenye utendaji. Hivyo, kila siku utapokea email moja inayokufundisha jinsi ya kutekeleza hatua husika. Mwisho wa siku, utakuwa umejijngea uwezo mkubwa wa kutumia Facebook kwa ajili ya biashara yako.

 Pia, washiriki wote watapata nafasi ya kuuliza maswali kwa email kwenda kwa wataalamu wetu kwa muda wote wa mafunzo bila gharama yoyote.

Mazingatio unapochagua mtoa huduma ya IT Tanzania

Katika maisha ya kiujasiriamali ya sasa, hauwezi kuepuka maumizi ya Tekinolojia.Tekinolojia siyo tu inakuwezesha kufikia watu wengi zaidi, bali pia kuongeza ubora na ufanisi wa huduma zako kitu kitakachokufanya uwe wa kipekee.

Wajasiriamali wengi wamekuwa na shauku na hamu kubwa ya kutumia tekinolojia ili kuongeza ufanisi wa huduma zao. Kwakuwa wengi wa wajasiriamali hawa hawana uelewa mkubwa wa mambo ya tekinolojia (na si kazi yao), hivyo hujitoa kafara kwa watu wa tekinolojia wakiamini wao ndiyo msaada wao mkubwa. Lakini si mara zote mambo yanaenda sawa.

Tangu kuanzishwa kwa Dudumizi Technologies, tumekuwa tukipokea wateja wengi ambao wamekuwa wakilizwa au kukatishwa tamaa na hawa watu wa tekinolojia. Hivyo ili kuwasaia wengine, katika makala hii, tutaangalia mambo muhimu ya kuzingatia pindi unapochagua mtoa huduma wa tekinolojia (IT).

Kufikia kikomo kwa Windows XP, nini athari zake kwa mtumiaji?

Mnamo tarehe 8/4/2014 kampuni ya utengenezaji wa mitambo endeshi ya kompyuta (Operating Systems) ya Microsoft ilisitisha utoaji wa huduma za muda mrefu kwa mitambo ya XP, ni moja ya mitambo endeshi inayotumika na watu wengi sana.Tangu kutoka kwa taarifa hizo, kumekuwa na maneno na mikanganyiko mingi mno kwa wateja hususan hapa Tanzania.

Kwakuwa ni mitambo inayotumika kwa weingi kwenye kompyuta nyingi zinazotumika kwenye mabenki na maofisini, hivyo watu walifika mbali hata kusema eti pesa zetu hazipo salama tena. Hivyo, ili kuondoa hofu hizi zinazoizunguka jamii, ungana nasi Dudumizi kwenye kujua nini maana ya kikomo hiki cha huduma na jinsi gani kinaweza kuathiri biashara yako?

Jinsi gani IT inaweza kuwasaidia SME

Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatilia matangazo ya kazi sehemu mbalimbali Tanzania, lengo langu kubwa halikuwa kwa ajili ya kutafuta kazi, bali nilitaka kujua uelekeo wa ajira kwa nchi yetu ya Tanzania. Kwani, uelekeo huu ndio utakaoweza kubadirisha mustakabali wa ufanisi wa kazi na maendeleo kwa taifa letu.Pia, nilitaka kujua je waajiri wanajua nani wanayemtafuta?


Mwaka juzi nilipata nafasi ya kuwa mmoja msemaji mkuu (Key note speaker) katika mkutano wa kimataifa juu ya E Commerce na E Governance ulioandaliwa na IEEE hapa China, hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuwa katika uwanja kama ule mbele ya magwiji toka makampuni makubwa duniani. Katika mkutano ule, nilizungumzia kuhusu aina mpya ya biashara ya online kwa kutumia mitandao jamii (Social Commerce), ni mada iliyovuta hisia za watu wengi sana hivyo ilikaribisha maswali mengi mno.


Moja ya swali nililoulizwa na Mr Jen Yao Chung toka kitengo cha tafiti cha IBM Marekani( IBM T.J Watson Research Center) ni jinsi gani tutaweza kupima faida au mchango wa mitandao jamii(social networks) kwenye biashara za mitandaoni(ecomerce). Katika kumjibu swali lake, nilimuambia kuwa, tunatakiwa kuifanya mitandao jamii(social networks) kuwa sehemu ya biashara ili tuweze kupima na kuuchunga mchango wake.

Baada ya kuisha kwa mkutano ule, nilikuwa na mengi ya kubadirishana na Mr Chung, nilimuuliza kwanini uliamua kuuliza lile swali, alinijibu kwa kusema, kwa muda mrefu, kumekuwa na utofauti kati ya muono wa mamanager wa IT juu ya nini wanatakiwa kufanya na nini wanachokifanya. Wengi wao wanadhani wao ni kwa ajili ya kutoa huduma (outputs) badala ya matokeo (outcomes), na hii ndio sababu inafanya makampuni mengi kutoona faida za moja kwa moja za IT, pia IT kushindwa kusukuma gurudumu la maendeleo ya kampuni husika.Hivyo alinisihi kutumia muda mwingi kufahamu uelekeo sahihi wa IT toka ule wa zamani uliozoeleka. Haswaa kwa sisi nchi zinzoendelea.

Connect With Us

 

New Project?

We do not just put codes to make a system, we help companies in their digital transformation challenges. We automate business process, workflows and communication.

Image